Mpigieni Mungu vigelegele, mshukuruni Bwana kwa mema yote x2
Sop: Msifuni kwa nyimbo zenye kupendeza, mwimbieni mtukuzeni milele x2
Alto: Msifuni Mungu wenu, mshangilieni, mwimbieni mtukuzeni milele x2
Tenor: Mtukuzeni, kwa nyimbo nzuri za shangwe, mwimbieni mtukuzeni milele x2
Bass: Msifuni kwa matendo yake makuu, mwimbieni mtukuzeni milele x2
Aliumba vitu vyote duniani, akatukabidhi sisi wanadamu Ni vyema tumshukuru Mungu wetu x2
Jua lachomoza kwa wakati wake, tunapata mwanga na joto mwilini Ni vyema tumshukuru Mungu wetu x2
Alipanga vyema majira ya mwaka, mvua hunyesha kwa wakati wake. (Ni vyema tumshukuru Mungu wetu x2)
Pepo zavuma kusini kaskazini, zavuma mashariki na magharibi (Ni vyema tumshukuru Mungu wetu x2)
Alipanga vilima na milima akapisha mito kwenye mabonde (Ni vyema tumshukuru Mungu wetu x2)
Comentários