Mpeni Mungu mali yake,Mpeni Bwana haki yake x2
Leteni zawadi kwa Bwana-
Mkate kiini cha ngano -
Divai tunda la mzabibu -.
Na Bwana atavipokea -
Na kazi za mikono yetu -
Nazo nafaka za mashamba
Nayo mapato ya mashamba
Na Bwana atayatakasa –
Sisi ni mali yake Bwana -
Toeni nafsi kwake Bwana –
Nayo furaha na uchungu
Na Bwana atavipokea –
Vitu vyote mali ya Bwana
Itangazeni sifa yake –
Uhubirini ukuu wake -
Milele hata na milele –
Comments