Mungu akaona si vyema mtu huyu awe peke yake Nitamfanyia mwenzake yule wanafanana naye Akaumba mwanamke, kamleta kwake mwanamume waishi pamoja
Mungu akawapa uwezo watawale viumbe vyote Mungu akasema zaeni muijaze dunia kwa watu Baraka za Mungu Baba, zimewashukia tangu leo zaeni matunda
Ewe mwanamume mpende mke wako kwa moyo wote Nawe mwanamke heshimu mume wako mtii daima, Ndoa ni maagano, kati ya watu wawili wapendanao
Nyumba yenu iwe hekalu lake Mungu kanisa ndogo Nyumba ya amani upole na furaha nyumba ya sala Mungu ameunganisha mwanadamu asitenganishe daima dawamu
top of page
bottom of page
Comentários