Mpaka lini Bwana, Utakaa mbali?
Kumetuchosha moyo kukawia hivi.
Utatujia lini, Ili tufurahi
Katika ile nuru, kuja kutukufu?
Mpaka lini Yesu, Utaacha watu
Uliowakomboa, Wawe na mashaka?
Wachache waamini, Kwamba utarudi;
Wachache wa tayari, Bwana kukulaki.
Waamshe watu wako, Tangaza kilio:
‘Mwe watakatifu, Bwanayu karibu!‘
Utatujia lini, Ili tufurahi
Katika ile nuru, Kutukufu?
Commenti