Moyo wako, Yesu mpendelevu, watuhurumia masikini;
Wawapokelea wakosefu, kwa msamaha, wema na amani.
Moyo hazina ya neema, utujalie daima!
Yesu twasalimu wako Moyo, twakushukuru kwa mapenziyo
Moyo makimbilio salama, takujalia japo wadhambi;
Tupokee leo kwa huruma, kasikilie yetu maombi!
Yesu utuhurumie, kwa wema tufanyizie,
Twataka kukutii daima, na kwako kupata usalama
Moyo ukashibishwa huzuni, kwa kutustahilia huzuni msamaha
Pia ukatiwa msalabani wa mbingu utupatie raha
Tufundishe leo pia, kukupenda kuzidia;
Donda lako utufungulie, kwako milele tukimbilie
Comments