top of page

Mlangoni pa Moyo

Mlangoni pa moyo; Mgeni! (Amesimama)

Amesimama pale, Mgeni! (Amesimama)

Umkaribishe sasa,

Umkaribishe Mwana

Wa Baba wa upendo: Mgeni! (Umkaribishe)


Moyo wako kwa Bwana, Fungua. (Fungulieni)

Asikuache mbali, Fungua. (Fungulieni)

Umkubali Rafiki,

Roho atafariji

Naye atakutunza: Fungua. (Fungukieni)


Usikie sauti Ya Bwana. (Uisikie)

Uyachague mambo Ya Bwana. (Mambo ya Bwana)

Ufungue mlango,

Usimwambie bado:

Jina lake tumai---- Yu Bwana. (Jina la Bwana)


Na ufungue moyo, Kwa Bwana (Fungulieni)

Utapewa msaada, Wa Bwana (Msaada wetu)

Uzuri utavikwa

Dhambi ataondoa,

Ukifungua moyo. Kwa Bwana (Fungulieni)

4 views0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page