Unakaribia wakati wa Kuja kwa Yesu.
Atawachukua watu wake Nyumbani juu.
Tunaiona mishale ya nuru Inayopenya giza;
Tunaiona mishale ya nuru Ya ufunuo.
Injili inatangazwa pote kwa mataifa;
Bwana wa Arusi atakuja Na tarumbeta.
Pamoja na malaika zake Bwana arudi,
Awapeleke waaminifu Wasife tena.
Wapenzi waliotengwa kale Watakutana;
Machozi yao wenye huzuni Yatafutika.
Comments