Bwana Bwana Bwana utuhurumie x2
Kristu Kristu (Kristu) utuhurumie x2
Bwana…………………
UTUKUFU
SA Utukufu kwa Mungu juu mbinguni
TB Na amani kote duniani
ALL Kwa watu wa mapenzi mema
Tunakusifu tunakuheshimu ,Tunkuabudu tunakutukuza x2
2. Twakushukuru Mungu kwa ajili,Ya utukufu wako mkuu ee Bwana,Ni wewe Mungu Mfalme wa mbinguni.
3. Baba Mwenyezi Bwana Yesu Kristu, Mwana wa pekee Mwana wa Baba,Mwana Kondoo Mwana wake Mungu.
4. Uondoaye dhambi za dunia,Utuhurumie tuhurumie,Maombi yetu Baba upokee.
5. Uketiye kuume kwake Baba, Utuhurumie tuhurumie, Ni wewe peke peke Mtakatifu.
6. Pekee yako Bwana pekee mkuu, Ewe Yesu Kristu pamoja naye,Roho Mtakatifu milele yote.`
NASADIKI- MILLENIUM
1. S/A- Nasadiki kwa Mungu mmoja- Nasadiki
T/B- Ndiye Baba yetu mwenyezi - Nasadiki
S/A- Muumba mbingu pia dunia - Nasadiki
T/B- Nasadiki kwa Yesu Kristu - Nasadiki (kweli)
Nasadiki, nasadiki ninasadiki x2
2. Mwana wa pekee wa Mungu
Aliyezaliwa kwa Baba
Akapata mwili kwa Roho
Kazaliwa naye Bikira
3. Kisha yeye kasulubiwa
Kwa amri yake Pilato
Kwa ajili yetu kateswa
Akafa na akazikwa
4 Kafufuka katika wafu
Akapaa juu mbinguni
Ameketi kuume kwake
Mungu Baba yetu mwenyezi
5. Ndipo atakapotokea
Kuhukumu wazima na wafu
Kwake Roho Mtakatifu
Kwa kanisa la Katoliki
6. Ushirika wa watakatifu
Ondoleo ya dhambi zetu
Nangojea ufufuko wa miili
Na uzima wa milele
MTAKATIFU : MILLENIUM
(Mtakatifu) Bwana Mtakatifu Bwana Mtakatifu Bwana Mungu wa majeshi
(Mbingu na du)nia mbingu na dunia Zimajaa utukufu wako
Hossana juu x3 Mbinguni x2
Mbarikiwa) yeye x2 yule mwenye kuja Kwa jina la Bwana x2
AMINA
Amina Amina Amina x2.
BABA YETU
Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe Ufalme wako utufikie utakalo lifanyike x2
1. Duniani kama mbinguni- Jina lako litukuzwe
Tupe leo mkate wetu
Mkate wetu wa kila siku
2.Tusamehe makosa yetu-
Kama vile twawasamehe
Wale waliotukosea
3. Situtie kishawishini
Walakini utuopoe
Maovuni utuopoe
4. Kwa kuwa ufalme ni wako-
Nguvu na utukufu pia
Utukufu hata milele
Comments