top of page

Mfalme yu Mlangoni

Mfalme yu mlangoni, Ndiye aliyetufia;

Mara wote wampendao atawakusanya.


Yuaja, yuaja, mlangoni anasimama;

Anakuja, anakuja, Kuja kwake karibu.


Dalili za kuja kwake Zinazidi kutimizwa;

Karibu wateule watamlaki Bwana.


`Sitafute duniani amani wala furaha,

Mpaka Bwana arudi dhambi kuondoa.


Tutakaa na Mwokozi Makaoni ya milele;

Daima tutafurahi kuwa watu wake.

7 views0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page