Mfalme wetu atuita tukae karamuni kwake;
Itakuwaje nasi kule Bwana ajapo?
Bwana ajapo, ndugu, Bwana ajapo!
Itakuwaje na sisi, Bwana akija?
Atavikwa vizuri sana, taji badala ya miiba;
Kweli tokeo la fahari Bwana ajapo.
Kwa furaha awakubali wenye mavazi ya arusi;
Tu wa heri tukimridhisha Bwana ajapo.
Kutakuwako na utengo: watalia waliomwasi;
Cha kutisha kitambo kile Kristo ajapo!
Mfalme utupe neema sisi tunapokungoja,
Tusiogope kukuona ujapo Bwana.
Comments