top of page

Mfalme Ajapo

Mfalme wetu atuita tukae karamuni kwake;

Itakuwaje nasi kule Bwana ajapo?


Bwana ajapo, ndugu, Bwana ajapo!

Itakuwaje na sisi, Bwana akija?


Atavikwa vizuri sana, taji badala ya miiba;

Kweli tokeo la fahari Bwana ajapo.


Kwa furaha awakubali wenye mavazi ya arusi;

Tu wa heri tukimridhisha Bwana ajapo.


Kutakuwako na utengo: watalia waliomwasi;

Cha kutisha kitambo kile Kristo ajapo!


Mfalme utupe neema sisi tunapokungoja,

Tusiogope kukuona ujapo Bwana.

4 views0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page