top of page

Meza Ipo Tayari


Meza yake Bwana ipo tayari, amekwisha andaa Bwana wetu Yesu, twende tukale chakula cha uzima x2

  1. Duniani hapa sisi tu wasafiri twaelekea kwake Mungu wetu, safarini twahitaji chakula hiki ili tupate nguvu za kutosha

  2. Tunapata neema tunaposhiriki meza yake Bwana kikamilifu, tujitayarishe basi tukampokee Bwana Yesu Kristu kwenye Ekaristi

  3. Mwili wake sio kama ile mana waliokula baba zetu jangwani, tule mwili na tunywe damu yake Yesu ili tupate uzima wa milele

  4. Tufungue mioyo tumkaribishe ili aingie ndani yetu, tutapata amani pia na furaha tukiwa naye Yesu kila wakati

2 views0 comments

Comentarios

Obtuvo 0 de 5 estrellas.
Aún no hay calificaciones

Agrega una calificación
bottom of page