Mapya ni mapenzi hayo,
Asubuhi tuonayo;
Saa za giza hulindwa,
Kwa uzima kuamka.
Kila saku, mapya pia,
Rehema, wema na afya,
Wokovu na msamaha,
Mawazo mema, furaha.
Tukijitahidi leo
Na mwendo utupasao,
Mungu atatueleza
Yatakayompendeza.
Mamboyetu ya dunia
Bwana atayang‘aria,
Matata atageuza
Yawe kwetu ya baraka.
Yaliyo madogo, haya
Bwana tukimfanyia,
Yatosha: tutafaidi
Huvuta kwake zaidi.
Ewe Bwana, siku zote,
Tusaidie kwa yote:
Mwendo wetu wote vivyo,
Uwe kama tuombavyo.
Comments