Umekuwa jasiri, jasiri jasiri sana
Tena hubabaishi, jasiri jasiri sana x2
Ulijipanga vema ukamfata dada yetu, tena bila aibu ukampa hayo maneno
Maneno matamu hayo (hayo maneno) ya mdomo wako (ni mazuri) maneno matamu hayo (hayo maneno) ya mdomo wako.
(T) Hayo maneno ____ maneno hayo ____ yamfariji___ maneno ya mdomo.
(B) Maneno
(T) Yampe raha ___ maneno hayo ____ maneno hayo ____ maneno ya mdomo.
1. Kuna wakati atanuna huyo, kuna wakati atakasirika huyo, ataacha kukusemesha huyo, labda pia utamuumiza huyo, (busara) busara yako (siku zote) siku zote ( mmh aaee) tumia mdomo wako umbembeleze (huyo mkeo) naye atafurahi sana kwa hayo maneno ___ (maneno)
2. Siku huwa hazilingani sana, kuna wakati mtagombana sana, anaweza akakukwaza sana, ila kumbuka unampenda sana, (busara)……….
3. Hakikisha unamjali huyo, hakikisha unamtunza huyo, hakikisha unamlinda huyo, wewe ndiwe heshima yake huyo, (busara...
Comments