Maria Maria Mama wa rehema sisi wanao twakuja kwako, wewe uliye tegemeo letu twakulilia utusikie, wewe ni mama mwaminifu mama mpole mama wa Mungu na kanisa lote x2
Wewe ni Mama wa shauri njema mama mpole tuombee kwa mwanao mkombozi wetu
Mama Maria kimbilio letu na kinga yetu pia yeye ni tulizo letu wanadamu
Una Baraka kutoka kwa Mungu naye Yesu mwana wako amebarikiwa
Sisi wanao tunakulilia tunakusihi sala zetu zifikishe kwa mwanao Yesu
Ulikingiwa dhambi ya asili ukamzaa mkombozi wa dunia Bwana Yesu Kristu.
Comments