Malaika kaleta Noeli ya kwanza, Kwa wachunga kondoo katika makonde, Bethlehemu wakawa walinzi wa zamu, Wakaona usiku ajabu ya nuru
Noeli, Noeli, Noeli, Noeli, Yesu yu Mungu na binadamu x2
Wakaona mbinguni, mwangaza wa nyota, Ing'aayo kwa mbali na masharikini, Wakaenda upesi, walivyoambiwa. Bethlehemu wamwone Mwokozi horini
Mashariki watoka wafalme watatu, Mamajusi waliotafuta mfalme, Wafuata hii nyota waliyoiona, Wasipate kumkosa wanayemtafuta
Kiongozi ni nyota iliyowaleta Hata mji wa Daudi alimozaliwa Ikakaa mara moja isiendelee Pale pale nyumbani alimo Mwokozi
Mamajusi walipoingia nyumbani Wakapiga magoti kwa heshima kuu Mara hiyo walipozifungua hazina Manemane, uvumba, dhahabu, watoa
Basi sisi wakristu na tumsujudie Tumhimidi Mwokozi, aliyeviumba Vitu vyote mbinguni duniani na sisi Na ametufia na kutukomboa
Comments