Leteni sadaka kamili ghalani x2 (Ili chakula kiwemo katika nyumba yangu, asema Bwana, Bwana wa majeshi) x2
Mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana, Nitafungua milango ya mbingu, asema Bwana Na kuwamwagia baraka tele, asema Bwana
Mimi ndimi mgawa wa vipaji, asema bwana, Nitawaongezea maarifa, asema Bwana Ya kuyashinda magumu yoyote, asema Bwana
Mtakachokiomba nitawapa, asema bwana, Nitawapa vyeo na mali nyingi, asema Bwana Nakuuondoa umasikini, asema Bwana
Nitawalinda na kuwasitawisha, asema Bwana, Nanyi mtazaa matunda bora, asema Bwana Yatakayo dumu milele yote, asema Bwana
Comments