Kristu ametii kwa ajili yetu hata kufa, kufa msalabani
1. Muwe na msimamo ule ule / aliokuwa nao Kristu Yesu.
2. Yeye kwa asili / alikuwa daima Mungu.
3. Yeye hakutaka kutumia usawa wake na Mungu / kwa kujifaidia mwenyewe.
4. Bali kwa hiari yake / aliachilia hayo yote.
5. Yeye akajitwalia/ hali ya mtumishi.
6. Akawa sawa na wanadamu / akaonekana kama mwanadamu.
7. Alijinyenyekeza na kutii mpaka kufa / hata kufa msalabani.
8. Kwa sababu hiyo / Mungu alimkweza juu kabisa.
9. Mungu alimpa jina lililo kuu zaidi / kuliko majina yote.
10. Ili kwa jina la Yesu / viumbe vyote vipige magoti.
11. Kila mtu akiri / ya kuwa Yesu Kristu ni Bwana.
12. Yeye ndiye Bwana / kwa utukufu wa Mungu Baba.
Comentarios