Utuhurumie
Bwana utuhurumie Ee Bwana x2
Bwana utuhurumie
Kristu utuhurumie Kristu utuhurumie x2,
(utuhurumie)
Bwana utuhurumie
UTUKUFU
Utukufu kwa Mungu juu mbinguni
na amani na amani Duniani Duniani kwa
kwa watu wenye mapenzi mema
Tunakusifu, tunakuheshimu,
twakuabudu, tunakutukuza
Twakushukuru, mfalme wa Mbinguni,
kwa ajili ya utukufu wako.
Ee bwana Mungu, Mfalme wa mbinguni,
Baba Mwenyezi, Muumba wa wote
Ee Bwana Yesu, Mwana wa pekee
Mwana kondoo, Mwana wake Mungu.
Uondoaye, dhambi za dunia,
tuhurumie, utuhurumie
Uondoaye, dhambi za dunia,
ulipokee, hili ombi letu.
Unayeketi kuume kwa Baba tuhurumie,
utuhurumie, Kwa kuwa wewe,
ndiwe peke yako, Mtakatifu,
peke yako Bwana
Peke yako mkuu, Bwana Yesu Kristu,
pamoja naye, Roho Mtakatifu
Kwa utukufu, wake Mungu Baba,
milele yote, Amina, Amina
NINASADIKI
Ninasadiki, ninasadiki, ninasadiki Ninasadiki, ninasadiki
Ninasadiki kwa Mungu mmoja, Baba mwenyezi muumba wa mbingu na vitu vinavyoonekana pia ambavyo
havionekani
Ninasadiki kwa Yesu Kristu,Mwana wa pekee
Mwana wake Mungu Mwanga kwa Mwanga na Mungu kweli,
Tangu milele atoka kwa Baba
Aliyezaliwa bila kuumbwa, mwenye umungu mmoja na Baba
Ambaye vitu vyote vimeumbwa naye, ameshuka toka mbinguni
Kwa ajili yetu sisi wanadamu, na kwa ajili ya wokovu wetu
Akapata mwili kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, kwake yeye
Bikira Maria akawa mwanadamu, akasulibiwa Pia kwa ajili yetu sisi, akateswa kwa mamlaka ya Ponsyo Pilato Akafa akazikwa
Akafufuka siku ya tatu kapaa mbinguni ilivyoandikwa Atarudi tena kwa utukufu kuwahukumuwazima na wafu
Ninasadiki pia kwa Roho, Mtakatifu, mleta uzima
Atokaye kwao Baba na Mwana, aliyenena, kwao manabii
Ninasadiki, kanisa moja, katoliki, hilo la mitume, Ninaungama na ubatizo, ufufuko na, uzima milele.
BABA YETU
Baba yetu uliye mbinguni Jinalo litukuzwe Baba yetu ufalme wako ufike (ewe Baba) Utusamehe makosa yetu Kama twawasemehe Baba na sisi wale watukoseao (ewe Baba)
Utakalo lifanyike duniani kama mbinguni
Utupe leo mkate wetu Mkate wa kila siku
Situtie katika vishawishi, Baba yetu
Lakini utuopoe Tuopoe maovuni
Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu
Na nguvu utukufu Utukufu hata milele
MWANA KONDOO
Mwanakondoo (mwana) wa Mungu
Uondoaye dhambi za dunia Utuhurumie, utuhurumie
Mwana mwanakondoo wa Mungu
Mwana kondoo - Wa Mungu wake Mungu
Mwanakondoo wa Mwana kondoo wake Mungu
Uondoaye dhambi za dunia
Uondoaye dhambi, dhambi za dunia
Uondoaye dhambi za dunia
Utujalie amani.
Comments