1. Kiongozi wangu Yesu niongoze mimi, niingie mlangoni mwako, nikayaone mema uliyoniahidi,kabla lango halijafungwa
Lango lile la mbinguni angalia mtumishi yule, lango lile (la mbinguni) kaza mwendo halijafungwa.
2. Ewe lango la mbinguni nakuomba Bwana, sasa unifungulie name, nipate kuingia hapo ulipo wewe, nifungulie kitini mwako
3. Ewe Bwana Mungu wangu ee Mwokozi wangu, unikumbuke enzini mwako, name nikaziimbe sifa zako milele, nifungulie kitini mwako
4. Ewe Roho Mfariji kiongozi wangu, mtuliza pia ya shidani, nipe uwezo wako nikimbilie enzi, bado lango halijafungwa
Comments