Kazi yangu ikiisha, nami nikiondoka,
Na kuvaa kutokuharibika,
Nitamjua Mwokozi nifikapo ng'amboni,
Atakuwa wa kwanza kunilaki.
Nitamjua , nitamjua nikimwona uso kwa uso,
Nitamjua,nitamjua kwa alama za misumari
Furaha nitapata nikiona makao
Bwana aliotuandalia
Nitamsifu Mwokozi kwa rehema na pendo
Vilivyonipa pahali Mbinguni
Naowaliokufa katika Bwana Yesu
nitawaona tena huko juu
Lakini nifikapo kwake huko Mbinguni
Nataka kumwona Mwokozi kwanza.
Milangoni mwa mji Bwana atanipisha
Pasipo machozi wala huzuni
Nitaimba wimbo wa milele; lakini
Nataka kumwona Mwokozi kwanza
Comments