top of page

Kazi Yangu Ikiisha

Kazi yangu ikiisha, nami nikiondoka,

Na kuvaa kutokuharibika,

Nitamjua Mwokozi nifikapo ng'amboni,

Atakuwa wa kwanza kunilaki.


Nitamjua , nitamjua nikimwona uso kwa uso,

Nitamjua,nitamjua kwa alama za misumari


Furaha nitapata nikiona makao

Bwana aliotuandalia

Nitamsifu Mwokozi kwa rehema na pendo

Vilivyonipa pahali Mbinguni


Naowaliokufa katika Bwana Yesu

nitawaona tena huko juu

Lakini nifikapo kwake huko Mbinguni

Nataka kumwona Mwokozi kwanza.


Milangoni mwa mji Bwana atanipisha

Pasipo machozi wala huzuni

Nitaimba wimbo wa milele; lakini

Nataka kumwona Mwokozi kwanza

22 views0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page