BWANA UTUHURUMIE.
Utuhurumie Ee Bwana, ee Bwana, ee Bwana
‘TuhurumieEe Bwana, ee Bwana, ee Bwana, Bwana, utuhurumie.
Utuhurumie, Ee Kristu
Utuhurumie, Ee Bwana
UTUKUFU
Utukufu juu kwa Mungu, utukufu juu mbinguni, na amani kote duniani kwa wenye mapenzi mema.
Tunakusifu, tunakuheshimu, tunakuabudu,tunakutukuza, twakushukuru kwa ajili ya utukufu wako mkuu.
Ewe Mungu ndiwe Mfame, wa mbinguni Baba Mwenyezi, ewe Bwana Yesu Kristu, wa pekee mwana wa Baba.
Ewe Yesu Mwanakondoo, wa Mungu mwana wa Baba, ewe mwenye kuziondoa dhambi zetu tuhurumie.
Ewe mwenye kuziondoa, za dunia dhambi za watu, ewe mwenye rehema nyingi, upokee maombi yetu.
Uketiye kuume kwake, Mungu Baba tuhurumie, kwa kuwa ndiwe uliye, peke yako Mtakatifu.
Peke yako ni wewe Bwana, peke yako Bwana mkuu, peke yako ni Mkombozi, peke yako Yesu Kristu.
Naye Roho Mtakatifu, katika utukufu wake, Mungu mmoja anayeishi, na kutawala milele yote.
NASADIKI: KARIOBANGI
1. Nasadiki kwa Mungu mmoja - Ninasadiki
Ndiye Baba yetu Mwenyezi- Ninasadiki
Muumba mbingu pia dunia - Ninasadiki
Nasadiki kwa Yesu Kristu
Nasadiki, nasadiki, ninasadiki ,Nasadiki, nasadiki, ninasadiki.
Mwana wa pekee wa Mungu- Ninasadiki.
Mwenye kuzaliwa kwa Baba- Ninasadiki
Akapata mwili kwa Roho- Ninasadiki
Kazaliwa naye Bikira - Ninasadiki
Kisha yeye kasulubiwa – Ninasadiki
Kwa amri ya Ponsyo Pilato- Ninasadiki
Kwa ajili yetu kateswa- Ninasadiki
Akafa na akazikwa- Ninasadiki
‘Kafufuka katika wafu- Ninasadiki
Kapaa juu mbinguni- Ninasadiki
Ameketi kuume kwake- Ninasadiki
Mungu Baba yetu Mwenyezi
Ndipo atakapotokea- Ninasadiki
Kuhukumu wazima na wafu- Ninasadiki
Kwake Roho Mtakatifu - Ninasadiki
Kwa kanisa la Katoliki
Ushirika wa watakatifu- Ninasadiki
Ondoleo la dhambi zetu- Ninasadiki
Nangojea ufufuko wa mwili- Ninasadiki
Na uzima wa milele
MTAKATIFU: KARIOBANGI
Mtakatifu, Mtakatifu, mtakatifu, Bwana Mungu wa majeshi
Mbingu na dunia zimejaa ‘tukufu wako.
Hosana - Hosanna juu mbinguni}
Hosana - Hosana juu mbinguni}x2
Mbarikiwa - Anayekuja kwa jina lake Bwana Mungu x2
FUMBO LA IMANI; KARIOBANGI
V. Fumbo la Imani
W. Fumbo la Imani Kristu alikufa
Fumbo la Imani Kristu alifufuka
Kristu atakuja tena x2.
BABA YETU
Baba Yetu uliye mbinguni Jina lako litukuzwe, Ufalme wako ufike utakalo lifanyike x2
Duniani kama mbinguni
Tupe leo mkate wetu
Mkate wetu wa kila siku
Tusamehe makosa yetu
Kama vile twawasamehe
Walio tukosea sisi
Situtie majaribuni.
walakini utuopoe
maovuni utuopoe
Kwa kuwa ufalme ni wako
Na nguvu na utukufu
Utukufu hata milele
MWANA KONDOO
Ee Mwana Kondoo
Uondoaye dhambi za dunia utuhurumie
Ee Mwana Kondoo
Uondoaye dhambi za dunia utuhurumie
Ee Mwana Kondoo
Uondoaye dhambi za dunia utujalie amani.
Comments