(Karibu, kwetu eh Masiya) Yesu eh Mwana wa Daudi.
(Karibu, na utukombowe) Yesu eh, twakungoja sana.
Emanueli, Mungu pamoja nasi, njoo Yesu uzima wetu x2
Tujalie roho wako, afariji na kuziongoza, nyoyo zetu kweli zaona kiu
(Karibu, kwetu eh Mwokozi wetu) Yesu eh mwana wa Daudi.
(Shujaa na mwenye uwezo) Yesu eh, twakungoja sana.
(Njoo kwetu mfalme wa Israeli) Yesu eh Mwana wa Daudi.
(Ya mbingu, mema tujalie) Yesu eh, twakungoja sana.
(Karibu na utuhifadhi) Yesu eh Mwana wa Daudi.
(Tulio wanyofu wa moyo) Yesu eh twakungoja sana.
(Karibu ujaze furaha) Yesu eh Mwana wa Daudi.
(Moyoni tujaze upendo) Yesu eh twakungoja sana.
Comments