top of page

Kaa Nami

Kaa nami, ni usiku tena;

Usiniache gizani, Bwana;

Msaada wako haukomi;

Nili peke yangu kaa nami.


Siku zetu hazikawi kwisha;

Sioni la kunifurahisha;

Hakuna ambacho hakikomi;

Usiye na mwiso, kaa nami.


Nina haja nawe kila saa;

Sina mwingine wa kunifaa;

Mimi nitaongozwa na nani

Ila wewe Bwana, kaa nami.


Sichi neno uwapo karibu;

Nipatalo lote si taabu;

Kifo na kaburi haviumi;

Nitashinda kwako kaa nami.


Nilalapo nikuone wewe,

Gizani mote nimulikiwe;

Nuru za mbinguni hazikomi;

Siku zangu zote kaa nami.

7 views0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page