Sitafuti mali, wala utajiri; Nataka kwa yakini nipate Mwokozi.
Chuoni mwa Ufalme, niambie Yesu,
Jina langu yakini limeandikwa, je?
Limeandikwa, je? Jina langu huko?
Kitabuni mbinguni, limeandikwa, je?
Dhambi zangu ni nyingi, ni kama mchanga,
Lakini damu yako, Mwokozi, yatosha;
Kwani umeahidi: zijapo nyekundu Zitakuwa nyeupe ilivyo theluji.
Mji mzuri sana, wa majumba makuu, Walipo malaika,
mji bila ovu;Wakaapo walio na mavazi safi,
Limeandikwa sasa, jina langu huko?
Comments