Jina lake Yesu tamu, Lihifadhi moyoni;
Litakufariji ndugu,Enda nalo popote.
Jina la Thamani,
(Thamani) (thamani)
Tumai la dunia
Jina la thamani - - tamu!)
Furaha ya mbinguni.
Jina la Yesu lafaa Kama ngao vitani.
Majaribu yakisonga, Omba kwa jina hili.
Jina hili la thamani Linatufurahisha,
Napotukaribisha, Na tunapomwimbia.
Mwisho wa safari yetu Tutakapomsujudu.
Jina hili tutasifu Furaha ya mbinguni.
Comments