Namwamini Mungu Baba Mwenyezi, Muumba mbingu na nchi:
Na Yesu Kristo Mwana wake wa pekee,
Bwana wetu, Aliyechukuliwa mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu,
Akazaliwa na Bikira Mariamu, akateswa zamani za Pontio Pilato,
Akasulibiwa, akafa, akazikwa, akashuka kuzimu;
Siku ya tatu akafufuka, akapaa mbinguni, ameketi mkono wa kuume wa Mungu Baba Mwenyezi: Kutoka huko atakuja kuwahukumu watu walio hai na waliokufa.
Namwamini Roho Mtakatifu: Kanisa Takatifu Katoliko:
Ushirika wa Watakatifu: Ondoleo la dhambi: kufufuliwa kwa mwili.
Na Uzima wa milele.
AMINA.
Commentaires