Huyu ndiye Yesu wa miujiza nauliza Huyu ndiye Yesu wa maajabu nauliza aliyegeuza maji kuwa divai Kwenye harusi kule Kana Galilaya
Huyu ndiye Yesu Mnazareti nauliza Huyu ndiye Mwana wa seremala nauliza aliyewaita wavuvi wa samaki Akawageuza wavuvi wa watu
Huyu ndiye Yesu mwenye huruma nauliza Huyu ndiye Yesu Simba wa Yuda nauliza aliyewakemea mapepo kwa nguvu Aliyewaamuru mapepo watoke
Huyu ndiye Yesu mwenye baraka nauliza Huyu ndiye Yesu mwenye chakula nauliza, aliyewalisha watu elfu tano Kwa mikate mitano na samaki wawili
Huyu ndiye Yesu mwenye vituko nauliza Huyu ndiye Yesu asiyeshindwa nauliza, aliyewatimua watu hekaluni Walipogeuza hekalu kuwa soko
Huyu ndiye Yesu mwenye hekima nauliza Huyu ndiye Yesu mwenye elimu nauliza, aliyeng'amua hila zake shetani Pale nyikani alipojaribiwa
top of page
bottom of page
Comments