top of page

Huniongoza Mwokozi

Huniongoza Mwokozi, ndipo nami hufurahi,

Niendapo pote napo, ataniongoza papo.


Kuongoza hunishika; kwa mkono wa hakika;

Nitaandamana naye Kristo aniongozaye.


Pengine ni mashakani nami pengine rahani;

Ni radhi, ijapo yote, yupo nami siku zote.


Mkono akinishika kamwe sitanung`unika;

Atakachoniletea ni tayari kupokea.


Nikiisha kazi chini sitakimbia mauti;

Kuishinda ni ya hakika nikiongozwa na Baba.

2 views0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page