Huniongoza Mwokozi, ndipo nami hufurahi,
Niendapo pote napo, ataniongoza papo.
Kuongoza hunishika; kwa mkono wa hakika;
Nitaandamana naye Kristo aniongozaye.
Pengine ni mashakani nami pengine rahani;
Ni radhi, ijapo yote, yupo nami siku zote.
Mkono akinishika kamwe sitanung`unika;
Atakachoniletea ni tayari kupokea.
Nikiisha kazi chini sitakimbia mauti;
Kuishinda ni ya hakika nikiongozwa na Baba.
Comments