Hubirini kwa sauti ya kuimba, tangazeni haya Hubirini kwa sauti ya kinanda, tangazeni haya Yatamkeni, tamkeni hadi mwisho wa dunia Semeni Bwana amelikomboa taifa lake
Mwimbieni Bwana wimbo ule mpya, mwimbieni Bwana enyi mataifa mwimbieni Bwana kwa sauti ya shangwe, Mwimbieni Bwana libarikini jina lake
Tangazeni wokovu siku kwa siku, hubirini habari za utukufu yahubirini mataifa sifa zake, na watu wote habari za ukuu wake
Mpeni Bwana utukufu na nguvu, mpeni Bwana enyi wana wa Mungu, pelekeni habari zake pande zote, Mpeni Bwana utukufu wa jina lake
Mwabuduni Bwana kwa utakatifu, tetemekeni mbeleze nchi yote semeni kwamba Bwana ametamalaki, atawahukumu watu wake kwa adili
Commentaires