top of page

Hima Hima Nanjongea



Hima hima leo, najongea kwako Bwana, Ninakuja kwako kwa unyenyekevu wangu, Nakuletea matunda ya jasho langu, Pokea Baba nami unipe Baraka) 2

  1. Kwa ukarimu nimejitolea mimi mwenyewe, Polepole nasonga mbele nifike kwako, Nikukabidhi nilicho nacho, hiki kidogo Baba pokea.

  2. Mapato yangu ni duni sana, we wanijua, Sina kitu kizuri cha kukuletea wewe, Nakukabidhi maisha yangu, uzima wangu Baba pokea.

  3. Mungu wangu ninakuja kwako nikushukuru, Umenilinda siku zote asante sana, Mavuno yangu nakupa wewe, na fedha zangu Baba pokea.

  4. Wiki nzima umenijalia uhai bure, Umenikinga na matatizo unanipenda, Mkate huu nakutolea, divai hii Baba pokea.

  5. Baraka zako ninazipokea siku kwa siku Mungu Baba nionyeshe Mbingu nifanye kazi, Mifugo yangu nakuletea, furaha yangu Baba pokea.

2 views0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page