top of page

Hii ni sauti

Hii ni sauti ya mtu yule, aliaye kutoka nyikani x2 Itengezeni njia ya Bwana,yanyoosheni mapito yake x2 Na wote wenye mwili watauona, wokovu wa Mungu aleluya x2

  1. Haya ng'oeni magugu yote, tusafishe tusafishe Haya ng'oeni na mizizi yake, tusafishe tusafishe (Tusaishe bila ya kinyongo, ndugu zangu tusafishe Tusafishe kwa moyo mmoja, ndugu zangu tusafishe)

  2. Tuichimbeni mizizi ya rushwa, tusafishe tusafishe Tuyafukieni mashimo ya rushwa, tusafishe tusafishe Tusafishe bila ya kinyongo, ndugu zangu tusafishe Tusafishe kwa moyo mmoja, ndugu zangu tusafishe

  3. Tujaze kifusi penye ubinafsi, tusafishe tusafishe Tujenge upendo kwa jamii yote, tusafishe tusafishe Tusafishe bila ya kinyongo, ndugu zangu tusafishe Tusafishe kwa moyo mmoja, ndugu zangu tusafishe

  4. Penye fitina tumwage Molami, tusafishe tusafishe Penye majungu tumwage Molami, tusafishe tusafishe Tusafishe bila ya kinyongo, ndugu zangu tusafishe Tusafishe kwa moyo mmoja, ndugu zangu tusafishe

  5. Tuzisafisheni nyumba za wachawi, tusafishe tusafishe Tuzisafisheni kwa jina la Mungu, tusafishe tusafishe Tusafisheni kwa imani, ndugu zangu tusafishe Tusafishe siku ile yaja, ndugu zangu tusafishe

  6. Tuing'oeni mizizi ya vita, tusafishe tusafishe Tupalilie shamba la upedo, tusafishe tusafishe Sisi sote ni watoto wa Mungu, ndugu zangu tupendane, Sisi sote baba yetu mmoja, ndugu zangu tupendane.

1 view0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page