Heri yangu ni kubwa mno, kwani nimebatizwa.
Mungu Mwenyezi mtukufu, kanifanya mwanae.
Aliyeniumba kwake, nitamwita Babangu,
Kuliko vyote nampenda, kwani ndiyo amriye.
Na mwenye kunikomboa, ndiye Mwana wa Mungu.
Rohoni mwangu daima, atakaa Roho yake.
Shetani naye namkana, nimfuate Mwokozi.
Mama wa Yesu Maria, atakuwa mamangu.
Vinitengavyo na Mungu, kweli navikana
Ninakuomba Yesu we’ nifikishe mbinguni.
Comments