top of page

Hatujui Saa

Hatujui sa-a ya kuja kwa Bwana,

Lakini dalili zasema karibu,

Atakaporudi, lakini kwa kweli,

Hatujui saa


Atakuja, kwa vile tukeshe;

Atakuja Mwokozi, Aleluya!

Atakuja kwa fahari ya Baba yake,

Hatujui saa.


Pana nuru kwao wapendao haki,

Pana kweli katika Chuo Cha Mungu;

Unabii hufundisha kuja kwake,

Hatujui saa.


Tutakesha tutaomba daima,

Tutafanya kazi mpaka akija;

Tutaimba na tutasoma ishara,

-Hatujui saa.

2 views0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page