top of page

Furaha kwa Ulimwengu

1. Furaha kwa ulimwengu!

Bwana amekuja;

Nyote mkaribisheni,

Mioyo yenu na mpeni;

(Wote wamshangilie)x2

Na wote, na wote wamshangilie.


2. Furaha kwake dunia!

Mwokozi ni Mfalme;

Bonde na mlima na mwamba,

Maji mitoni na shamba,

(Rudisheni sauti) x2,

Rudisheni, na rudisheni sauti.


3. Dhambi zisiongezeke,

Wala wahalifu;

Yuaja kutubariki,

Atuletea ushindi;

(Kuharibu dhambi,) x2

Na kuharibu, na kuharibu dhambi.


4. Atawala na neema,

Kwao mataifa;

Utukufu na waone,

Haki yake itendeke;

(Kwa upendo wake,)x2

Kwa upendo, na kwa upendo wake.

0 views0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page