top of page

Furaha

Furaha tutakapofi-ka huko, pamoja na ma-laika, mbinguni kweli furaha.

Makao, ya Mungu Baba mbinguni, alipo Yesu Mkombozi, na pia mfalme mbinguni.

Shida nyingi za dunia, mateso ya kila siku, yataisha milele tuingiapo mbinguni,

Shangwe, vigelegele, kote zitasikika, karamuni ya wateule wake Bwana.


Wakristu, tusipotubu amini, kamwe hatuta-ingia haya makao mbinguni.

Na pia, tusipofwata kamili, injili yake Mwokozi, hatutafika mbinguni.

Na furaha ni kwa wale, wenye wema na imani, katika mambo yote, yampendezaye Mungu.

Hawa wataalikwa, hawa watapokea, taji lao la utukufu wa milele.


Tusiwe kama wana I-sraeli, waliovunja agano lao na Mungu muumba.

Walipo tenda maovu hakika, bila majuto moyoni, mbele za macho ya Bwana.

Mungu aliwatendea, sawa na matendo yao, kawafanya watumwa, wasio hata na haki,

Hivyo matendo yetu, pia maneno yetu, yawe sawa na imani ndani ya Kristu.


Eeh Ndungu, ee dada yangu sikia, ni heri tanga-za leo, msimamo wa maisha.

Tazama, siku Karibu yafika, atakaporudi tena, Yesu na kutuhukumu.

Jiepushe na madhambi, na anasa za dunia, ole watenda dhambi, atawatupa motoni,

Wenye matendo mema, atawakaribisha, kwenye karamu ya mbinguni kwa furaha.

0 views0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page