BWANA ‘TUHURUMIE’
Bwana tuhurumie, Bwana tuhurumie, Bwana tuhurumie ee Bwana, ee Bwana…
Kristu tuhurumie, Kristu tuhurumie ,Kristu tuhurumie ee Kristu, ee Kristu tuhurumie
Tuhurumie;
Bwana tuhurumie……… (endelea kama mwanzo)
UTUKUFU
1. Tenor: Kwake utukufu Mungu juu mbinguni,
Sop: Na kote amani hapa duniani
Wote: Kwa wote watu wa mapenzi mema).
Sop/Alto: Tunakushukuru Mungu kwa ajili
Wote: Ya utukufu wako ule mkuu.
KIITIKIO: Tunakusifu, (Bwana) tunakuheshimu, tunakuabudu (Bwana) tunakutukuza.x2
2. Tenor: Ewe Bwana Mungu Mfalme wa mbinguni,
Wote: Ni wewe Mungu Baba Mwenyezi
Sop/Alto: Bwana Yesu Kristu Mwana wa pekee
Wote: Ee Bwana Mungu Mwana wa Baba.
3. Tenor: Mwenye kuondoa dhambi za dunia,
Wote: Ee Bwana Yesu utuhurume.
Sop/Alto: Mwenye kuondoa dhambi za dunia,
Wote: Ee Yesu we pokea ombi letu.
4. Tenor: Mwenye kuketi kuume kwa Baba,
Wote: Wetu Mwokozi utuhurumie.
Sop/Alto: Pekee yako Bwana ndiwe Mtakatifu,
Wote: Na pekee yako mkuu Yesu Kristu.
5.Tenor Pamoja na yeye Roho Mtakatifu,
Wote: Kwa utukufu wake Mungu Baba.
Sop/Alto Pamoja na yeye Roho Mtakatifu,
Wote: Kwa utukufu wake Bwana Baba.
NASADIKI
1. Tenor: Nasadiki kwa Mungu mmoja kwa Mungu mmoja, muumba mbingu na dunia na kwa Mwana wa pekee, Yesu Kristu
Bwana wetu, ( Nasadiki) Alitungwa kwa uwezo wake Roho Mtakatifu, kazaliwa na Bikira.
Kiitikio: (T) Nasadiki. (W) Nasadiki –I Kweli nasadiki.
2. Aliteswa kwa Pilato pia alisulibiwa, na akafa akazaliwa, akazikwa, kashukia na kuzima kafufuka yeye siku ya tatu toka kwa
wafu.
3. Akapaa juu mbinguni ameketi kuume kwake Baba Mwenyezi, atakapotokea kuhukumu watu wote wazima na wafu.
5. Nasdiki kwa Roho Mtakatifu na kanisa takatifu katoliki la mitume, ushirika ule mwema wa watakatifu wote, maondeleo ya
dhambi zetu, ( ufufuko wa miili na uzima wa milele, ijayo A-mina) x 2
MTAKATIFU
Mtakatifu (Mtakatifu)Mtakatifu Bwana Mungu wa majeshi
Mbingu na dunia, mbingu na dunia kweli zimejaa utukufu wako.
Hosanna juu Hosana juu mbinguni, Hosanna juu Hosana juu mbinguni x2
Mbarikiwa anayekuja, na kwa jina lake Mungu wa majeshi x 2
FUMBO LA IMANI
Ee Bwana-a -kila tunapo kula mkate huu, na kunywa kikombe hiki, Tunatangaza kifo chako-o
mpaka utakapo kuja .
BABA YETU
Baba yetu wa mbinguni jina lako litukuzwe, ufalme wako na, ufike utakalo lifanyike x 2
1. Duniani kama mbinguni- Baba ee Baba yetu;
Tupe leo mkate wetu……. Mkate wetu wa kila siku……..
2. Tusamehe makosa yetu……. Kama vile twawasamehe ……… waliotukosea sisi
3. ……. Situtie kishawishini…….. walakini utuopoe…….. maovuni utuopoe……..
4. Kwa kuwa ufalme ni wako….. na nguvu na utukufu….. utukufu hata milele…..
MWANAKONDOO WA MUNGU
Mwanakondoo wa Mungu, uondoaye dhambi za dunia, tuhurumieutuhurumie x 2
Comments