1. Ekaristia takatifu ni mwili na damu yake Yesu, aliyesulubiwa msalabani ili kutukomboa, jioni alhamisi katwaa mkate (pia) divai kawapa wanafunzi (ili) wanywe kwa ukumbusho wake.
Njooni njooni wateule (wote) tumwambudu Kristu katika sacramenti (ndugu) njooni njooni tumwabudu Yesu, njooni njooni tumwabudu Kristu katika sacramenti.
2. Tujongee taratibu tukale karamu takatifu, aliyotuachia Yesu Kristu kwa ukarimu wake, chakula cha uzima (na) kinywaji cha roho (hili) ni fumbo alituachia tuadhimishe kwa ukumbusho wake
3. Ekaristi takatifu huleta neema ya mbinguni, huleta mapatano kati yetu naye muumba wetu, walio na Imani wanayo baraka (hadi) milele wanalo hakikisho (lile) la kushiriki kwa utukufu wake.
Comentários