(Ee Mungu Baba upokee sadaka, sadaka safi isiyo na doa, ni sadaka yake mwanao mpenzi
uliyependezwa naye )x2
1. Ni ajabu ya sadaka hii, mkate kugeuzwa mwili wake Yesu, na divai kugeuzwa damu yake
2. Ni sadaka ya agano jipya, sadaka ya Bwana wetu Yesu Kristu, iliyotolewa ili tuokoke
3. Mungu Baba tunakutolea, sadaka yetu hii kama ukumbusho, wa sadaka aliyoitoa Yesu
4. Sisi twaja hapa mbele yako, tukiwa na sadaka zetu mbalimbali, twakusihi Baba yetu zipokee.
Comments