Ee mpendwa wa nafsi yangu, usimame nawe ujipambe, mavazi yako mazuri (kisha) twende hekaluni nikathibitishe kwamba mimi nakupenda
Duniani kuna mambo, kuna wengi kuna mengi
Kati yao wengi nayo mengi mimi nimekuchagua wewe.
Duniani kuna mambo, kuna shida kuna raha
Wakati wa dhiki na raha mimi nitakuwa mfariji.
Duniani kuna mambo, kuna kupeana kero,
Wakati wa penzi na mashaka mimi nitakuwa mwaminifu.
Duniani kuna mambo, kuna wengi mwafanana,
Kiapo nilicho apa leo mimi ndiyo hukumu yangu.
Comments