Ee Bwana sistahili, sistahili ee Bwana uje moyoni mwangu x2 (Lakini) sema neno (moja) sema neno (moja tu) nami nitajongea mbele kwa karamu.
Karamu ya Bwana yatupa uzima, ni mwili wa Bwana na damu yake.
Hiki ni chakula, kutoka mbinguni, Bwana atuita kutushibisha.
Huu mwili wangu, hii damu yangu, njoni kwangu nami nitawalisha.
Siku zote Bwana, atulisha sisi, kwa chakula bora kutoka mbinguni.
Atukuzwe Baba, atujalie, uzima tukila chakula hiki.
Comments