Ee Bwana twakuomba upokee vipaji vyetu x2,
hivyo vyote ni mali yako tumepata kwa wema wako pokea x2
Mkate divai twakutolea
Twakuomba Baba upokee
Mazao ya mashamba twakutolea
Twakuomba Baba uyabariki
Pokea nazo nyoyo zetu
Pokea Baba twakuomba
Na fedha za mifuko twakutolea
Twakuomba Baba tubariki
Na kazi za mikono twakutolea
Twakuomba Baba zikupendeze
Furaha na uchungu twakutolea
Twakuomba Baba upokee.
Comments