top of page

Chini ya Msalaba

Chini ya msalaba Nataka simama;

Ndio mwamba safarini, Wa kivuli chema;

Ni kweli kwa roho yangu Ni tuo kamili,

Tatua mzigo wangu Wakati wa hari.


Hapa ni pema sana, Ni ngome kamili;

Hapa yameonekana, Mapenzi ya kweli;

Kama alivyoonyeshwa Yakobo zamani.

Msalaba umekuwa Ngazi ya mbinguni.


Na Yesu Msalabani Walimkemea,

Alikufa niokoke Niliyepotea:

Naona ajabu sana Ya mambo mawili

Jinsi alivyonipenda Nisiyestahili.


Atakayeonana Na Yesu mbinguni,

Njia yake aanzapo Ni Msalabani;

Wokovu upo hapa tu, Mwingine hapana.

Kisha kuna furaha kuu Pamoja na Bwana

7 views0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page