Cha kutumaini sina, ila damu yake Yesu,
sina wema wa kutosha, dhambi zangu
kuziosha, kwake Yesu nasimama
Ndiye mwamba ni salama x3
Njia yangu iwe ndefu, yeye hunipa wokovu
Mawimbi yakinipiga, nguvu zake ndizo nanga
Kwake Yesu nasimama
Ndiye mwamba ni salama x3
Nikiitwa hukumuni, rohoni nina amani
Nikivikwa haki yake, sina hofu mbele
zake, kwake Yesu nasimama
Ndiye mwamba ni salama x3
Damu yake na sadaka, nategemea
daima, yote chini yakiisha, Mwokozi
atanitosha, kwake Yesu nasimama
Ndiye mwamba ni salama x3
Comments