Utuhurumie ee Bwana, ee,
Ee Bwana, ee Bwana
Utuhurumie ee Bwana, ee,
Ee Bwana, ‘tuhurumie.
Utuhurumie ee Bwana, ee,
Ee Bwana, ee Bwana
Utuhurumie ee Bwana, ee,
Ee Bwana, ‘tuhurumie.
Ee Kristu, ‘tuhurumie, ‘tuhurumie,
Utuhurumie ee, ee Kristu ‘tuhurumie,
Ee Kristu ‘tuhurumie.
Utuhurumie…
UTUKUFU
Utukufu kwa Mungu juu mbinguni, Na amani iwe kwa watu wenye Mapenzi mema duniani kote.
Tunakusifu, Tunakusifu, tunakuheshimu, tunakuabudu,
tunakutukuza.
Tunakushukuru, Mungu kwa ajili, Ya ‘tukufu wako mkuu, ee Bwana, ni Mungu ndiwe Mfalme wa mbinguni
Ee Baba Mwenyezi, Bwana Yesu Kristu, Ee Mwana wa pekee, ee Mungu Mwana Kondoo wa Mungu, Mwana wake Baba.
Mwenye kuondoa dhambi za dunia, Utuhurumie, ‘tuhurumie,
Maombi yetu, Bwana, uyapokee.
Mwenye kuketi kuume kwa Baba, Utuhurumie, kwa kuwa ndiwe
Pekee yako ni Mtakatifu
Pekee yako, Bwana, pekee yako mkuu, Ewe Yesu Kristu, pamoja naye Roho Mtakatifu milele yote.
NASADIKI
Nasadiki kwa Mungu Mmoja- Nasadiki
Ndiye Baba yetu Mwenyezi- Nasadiki
Muumba mbingu pia dunia- Nasadiki
Nasadiki kwa Yesu Kristu- Nasadiki
Nasadiki Nasadiki (Nasadiki) Nasadiki, Nasadiki.
Mwana wa pekee wa Mungu- Nasadiki
Aliyezaliwa kwa Baba- Nasadiki
Akapata mwili Roho- Nasadiki
Kazaliwa naye Bikira- Nasadiki
Nasadiki Nasadiki (Nasadiki) Nasadiki, Nasadiki.
Kisha yeye ‘kasulibiwa- Nasadiki
Kwa amri ya Pilato-Nasadiki
Kwa ajili yetu ‘kateswa- Nasadiki
Akafa na akazikwa- Nasadiki
Nasadiki Nasadiki (Nasadiki) Nasadiki, Nasadiki.
‘Kafufuka katika wafu- Nasadiki
Akapaa juu mbinguni- Nasadiki
Ameketi kuume kwake- Nasadiki,
Mungu Baba wetu Mwenyezi- Nasadiki,
Nasadiki Nasadiki (Nasadiki) Nasadiki, Nasadiki.
Ndipo atakapotokea- Nasadiki
Kuhukumu wazima na wafu-Nasadiki,
Kwake Roho mtakatifu-Nasadiki
Kwa kanisa la katoliki- Nasadiki
Nasadiki Nasadiki (Nasadiki) Nasadiki, Nasadiki.
Ushirika wa watakatifu- Nasadiki
Ondoleo la dhambi zetu- Nasadiki
Nangojea ‘fufuko wa mwili- Nasadiki
Na uzima wa milele- Nasadiki
MTAKATIFU
Mtakatifu, mtakatifu,
Mtakatifu, Bwana Mungu.
Mtakatifu, mtakatifu,
Mtakatifu Bwana Mungu, wa majeshi, x2
Mbingu na dunia zimejaa utukufu
Mbingu na dunia, mbingu na dunia,
Mbingu na dunia zimejaa utukufu wako,
Zimejaa utukufu wako.
Hosana juu, hosanna juu,
Hosana juu, hosanna juu mbinguni x2
Mbarikiwa yeye ajaye kwa jina
Mbarikiwa yeye, mbarikiwa yeye,
Mbarikiwa yeye ajaye kwa jina la Bwana,
Ajaye kwa jina la Bwana.
Hosana juu, hosanna juu,
Hosana juu, hosanna juu mbinguni x2
FUMBO LA IMANI
Yesu Kristu alikufa
Yesu Kristu alikufa,
Yesu Krisu alifufuka
Yesu Kristu atakuja kwetu tena x2
BABA YETU
Baba yetu wa mbinguni, (Baba),
Jina lako litukuzwe, ufalme wako ufike,
(Baba) utakalo lifanyike}x2
Duniani kama mbinguni, Baba- Utakalo lifanyike
Tupe leo mkate wetu, Baba- Utakalo lifanyike
Mkate wetu wa kila siku, Baba- Utakalo lifanyike
Tusamehe makosa yetu kama vile tunavyo wasamehe waliotukosea sisi- Utakalo lifanyike.
Situtie kishawishini, Baba -
Walakini utuopoe, Baba -
Maovuni utuopoe,Baba -
Kwa kuwa ‘falme ni wako, Baba -
Na nguvu na utukufu, Baba -
Utukufu hata milele, Baba
MWANA KONDOO
Ee Mwana kondoo wa Mungu
Uondoaye dhambi za dunia, ee
Ee Mwana ‘tuhurumie.
Mwana kondoo wa Mungu, ee,
Ee Mwana. ‘tuhurumie. x2
Mwana kondoo wa Mungu, ee , utujalie
Mwenye kuondoa dhambi zetu, ee
Amani utujalie, utujalie amani, ee
Amani utujalie, utujalie, ee,
Amani utujalie.
コメント