Bwana Yesu asema… mimi ndimi mkate wa uzima, yeye ajaye kwangu hataona njaa, naye aniaminiye hataona kiu.
Ewe Yesu Kristu Bwana wa utukufu wewe ndiwe chakula na pia ni kinywaji tushibishe kwa Mwili na Damu yako
Mwili wako Bwana ni chakula cha kweli, Damu yako Yesu ni kinywaji cha uzima utulishe pia Bwana utunyweshe.
Ekaristi Bwana ni uzima wa Mbingu, ulituachia siku ile ya karamu tufanye hivyo kwa ukumbusho wako.
Commentaires