Nakaza mwendo mbinguni, kila siku napanda juu;
Naomba nikisafiri, ‘Bwana uniongoze juu.‘
Bwana uniinue juu Kwa imani hata mbingu.
Juu kuliko dunia; Bwana uniongoze juu.
Moyo wangu hautaki Kukaa palipo shaka;
Wengine wapenda chini Nia yangu ni kupanda.
Nataka kupanda juu Nisishindwe na adui;
Kwa imani nasikia Sauti ya washindaji.
Kupanda juu nataka Niuone utukufu;
Hata mwisho nitaomba, ‘Bwana uniongoze juu.‘
Comments