Bwana ni kinga na ngome yangu Bwana ni mwamba na ngao yangu. (Katika shida nisadie katika tabu uniokoe ni wewe uliye mlinzi wangu x2
Katika hofu unitulize, Ee Bwana wangu ee Mungu. Shetani mwovu asinishinde, nilinde Bwana nisipotee.
Pasipo wewe niko dhaifu, pasipo wewe sifai kitu. Nilinde Bwana nikinge Bwana, nisianguke katika dhambi.
Unipe nguvu ee Mungu wangu, unipe nguvu niwe imara. Unijalie Rehema zako, unijalie fadhili zako.
Comments