Ninakuja kwako Bwana – Bwana nipokee x 2
Nakuabudu Bwana (Kwa sala na) kwa nyimbo x 2,
Bwana nitakase mimi Bwana niokoe x 2
1. Wewe ndiwe kinga yetu-wewe ndiwe nguvu,
Wewe ndiwe muumba wetu -wewe ndiwe Bwana.
2. Wewe ndiwe Bwana wa majeshi -mfalme wa mbinguni
Ndiye Mungu mwema Mungu kweli -apendaye haki
3. Jina lako litukuzwe-mfalme wa mbinguni
Wewe ndiwe Bwana mtakatifu -Mungu wa neema.
4. Atukuzwe Mungu Baba- Pia na mwana,
Pamoja na Roho mtakatifu- Milele Amina.
Comentarios