Bwana ninakuhitaji! Nimpofu, maskini;
Unishike mkononi, Kwako napata nguvu.
Kila saa, kila saa Bwana ninakuhitaji;
Kila saa, kila saa, Unilinde kila saa.
Univike na mavazi Ya usikivu wako;
Nguo zangu ni machafu, Nazitamani zako.
Wewe ukiniongoza Nitakwenda salama;
Nenda nami siku zote, U nuru na uzima.
Na ikiwa m-beleni Sehemu yangu ngumu,
Au ikiwa furaha, Unilinde kila saa.
Comments