top of page

Bwana ni Mchunga

Bwana ni Mchunga, Sitahitaji;

Majani mabichi malisho yangu.

Ananinywesha maji matulivu;

Atanirudisha nikipotea.


Nipitapo bondeni mwa mauti

U mlinzi wangu sitaogopa;

Fimbo lako latosha kunilinda;

Ukinifariji sina hasara.


Kati ya mateso meza waandaa,

Na kikombe changu kinafurika;

Umenipaka kichwani mafuta;

Nitaulizaje zaidi kwako?


Wema na fadhili zinifuate

Siku zangu zote hata milele;

Nami nitakaa nyumbani mwa Bwana

Katika ufalme wa pendo lake.

1 view0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page